Thursday, August 29, 2013

Kundi la kifo Uefa Champions League


Upangaji wa makundi ya michuano ya Uefa Champions league unafanyika baadaye leo huku tayari timu zikiwa zimewekwa kwenye makundi manne yanayoweza kutoa sura ya timu gani inaweza kupangwa na timu gani kwenye hatua ya makundi lakini wengi wakijiuliza nani ataangukia kundi la kifo.

Manchester City inaweza kuangukia kundi moja na Bayern Munich, Atletico Madrid au Paris Saint-Germain, na Napoli.

Lakini Chelsea, Manchester United na Arsenal wako katika hatari ya kuangukia kwenye kundi la kifo na wanaweza kujikuta wapo kundi moja na Atletico au PSG, Borussia Dortmund na Napoli.

Kesi mbaya kwa Barcelona na Real Madrid watajikuta mmoja wao anaangukia kwenye kundi moja na PSG, Man City au Borussia Dortmund, na Napoli.

Hivi ndivyo timu zilivyogawanywa kwenye makundi na zimepangwa kwa kutegemea kile walichokifanya kwenye mashindano ya Ulaya katika kipindi cha miaka mitano.

Pot One: Bayern Munich, Barcelona, Chelsea, Real Madrid, Manchester United, Arsenal, FC Porto, Benfica.
Pot Two: Atletico Madrid, Shakhtar Donetsk, AC Milan, Schalke, Marseille, CSKA Moscow, PSG, Juventus
Pot Three: Zenit, Man City, Ajax, Borussia Dortmund, Basel, Olympiakos, Galatasaray, Leverkusen
Pot Four: FC Copenhagen, Napoli, Anderlecht, Celtic, Steaua Bucuresti, Viktoria Plzen, Real Sociedad, Austria Vienna

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.