Thursday, August 22, 2013

Chelsea vs Aston Villa

 
Chelsea usiku wa kuamkia leo ilifanikiwa kuzoa pointi nyingine tatu za ligi kuu ya England EPL baada ya kuichapa Aston Villa kwa mabao 2-1 mchezo uliopigwa darajani Stamford Bridge.

Chelsea walitupia mabao yao kupitia kwa kipa wa beki wa Aston Villa aliyejifunga na bao la pili likitupiwa wavuni na Ivanovic huku lile la Aston Villa likifungwa na Benteke.
Kocha wa Chelsea Jose Mourinho na yule wa Aston Villa Paul Lambert walitupiana vijembe baadaye huku Mourinho akimtaka Lambert kuonesha kuwa amekuwa wakati alipokuwa akijaribu kupinga kila maamuzi ya mwamuzi.

Ivanoviv na Benteke walisalimika kutolewa nje kwa kadi nyekundu wakati Ivanovic alipompiga kiwiko Benteke ambaye naye baadaye alirudisha kupiga kiwiko na mwamuzi akamuonya.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.