Friday, August 9, 2013

KISU SHINGONI : Suarez huzuni,PFA yashindilia kisu kingine


Boss wa Chama cha wachezaji wa kulipwa PFA,Gordon Taylor ameshindilia kisu akisema mshambuliaji Luis Suarez hawezi kuihama Liverpool katika muda uliobaki.

Suarez, 26,ametakiwa kufanya mazoezi ya peke yake baada ya kulazimisha kutaka kuondoka kwenye timu hiyo huku ofa mbili za Arsenal zikichomolewa.
 
Taylor anasema kuna ugumu kwa Suarez kuondoka kulingana na muda mfupi uliobakia kwa klabu hiyo kuweza kuziba pengo lake na ugumu unaokuja sit u kumuuza kwa washindani wao lakini kuziba nafasi yake kwa uhalisia ni vigumu. 

Mmiliki wa Liverpool John W Henry tayari amesema kuwa Suarez hawezi kuuzwa wakati huu wa maajiraa ya joto.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.