Tuesday, January 28, 2014

Cech ampeleka Diego Costa Chelsea

Ni kama golikipa Petr Cech wa Chelsea amempeleka mshambuliaji wa Atletico Madrid Chelsea baada ya golikipa wa Chelsea anayecheza kwa mkopo Atletico Madrid Thibaut Courtois kuhofia bench akiorudi kwenye timu hiyo na sasa anatumika kama chambo.

Chelsea na Atletico Madrid zinaelezwa kuwa zimefikia makubaliano ya kubadilishana wachezaji hao deal itakayomfanya Diego Costa kutua Stamford Bridge msimu ujao na Courtois kubakia Atletico,hii ni kwa mujibu wa media za Hispania.

Costa ametumbukia wavuni mara 19 msimu huu katika La Liga na hesabu kubwa za kocha wa Chelsea Jose Mourinho ni kunasa mshambuliaji.

Chelsea walimtaka Courtois kusaini mkataba mpya licha ya kwamba hajawahi kucheza kwenye timu hiyo lakini kipa huyo ameomba asajiliwe moja kwa moja Atletico

Awali Courtois alisema atarudi Chelsea endapo atakwenda kuwa golikipa chaguo la kwanza mbele ya Petr Cech kwasababu hawezi kwenda kwenye timu ambayo atasugua benchi,kwake kubwa ni kucheza iwe Chelsea au klabu nyingine.



Cabaye rasmi wa PSG

Newcastle na Paris St-Germain wamefikia makubaliano kwa kiungo Yohan Cabaye kwa dau la paundi milioni 20.

PSG Jumapili walitoa ofa ya paundi milioni 14 ikapigwa chini na Newcastle lakini sasa makubaliano yamefikiwa kwa dau la paundi milioni 19 ambalo linaweza kuongezeka kufikia paundi milioni 20.

 Cabaye in the Premier League
  • 2013-14: 19 apps, seven goals
  • 2012-13: 26 apps, six goals
  • 2011-12: 34 apps, four goals

Monday, January 27, 2014

Sakata la Owino Logarusic bado tata


Huko kwa Wekundu wa Msimbazi Simba licha ya kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Rhino Rangers kwenye mchezo wa ligi kuu hapo jana,hali ya mambo si shwari baada ya kocha wake Zdravko Logarusic kugomea beki Joseph Owino kujumishwa kikosini.

Suala hilo la Owino linaonekana kuwavuruga baada ya kutibuana na Loga mazoezini na kwenye mchezo wa jana hakuwepo kabisa kikosini.

Suala hilo pia limeonekana kuwagawa viongozi wa Simba ambao bado wanaona Owino ana umuhimu mkubwa kwenye kikosi hicho hasa sehemu ya ulinzi.

MJUMBE KAMATI YA UTENDAJI
Mmoja wa wajumbe wa kamati ya utendaji aliyezungumza na supermariotz kwa masharti ya kutotajwa jina amesema wazi kuwa kocha huyo huenda akaondoka Simba mapema zaidi kwasababu ya msimamo aliouweka kwenye suala hilo.

"Unajua tulijaribu kumuombe msamaha Owino baada ya kutibuana na kocha mazoezini lakini kocha ameonesha msimamo anasema tuchague Owino awe nje ya timu yeye abaki ndani au yeye aondoke na Owino arudi kwenye timu sasa hili linatuweka njia panda,japo tunatambua mchango wa Owino na tunamuhitaji"Alisema mnyetishaji huyo kutoka kamati ya utendaji.

Amesema inawezekana kocha huyo akawa na muda mfupi wa kukaa Simba hasa kwasababu ya tabia zake za kuwatukana wachezaji mazoezini kama ilivyotokea kwa Owino na kutokubali ushauri.

MATOLA ABANWA
Kocha msaidizi wa Simba Suleima Matola akabanwa kuhusu suala la Owino akasema hawezi kuzungumza suala hilo kwa upana kwakuwa liko juu ya uwezo wake lakini anachojua ni kwamba Owino alitofautiana na kocha Logarusic kwenye mazoezi na ndio sababu ya kutokuwepo kambini wakati wakifanya maandalizi kwenye mchezo wa jana dhidi ya Rhino Rangers.

WANACHAMA WAKATIA NENO
Wanachama wa klabu hiyo nao baada ya mechi dhidi ya Rhino Rangers kwenye mkusanyiko wa vikundi kila mmoja alikuwa akisema lake kuhusiana na Owino na kocha Logarusic.

Wengine wamemuunga mkono Loga wakisema ni kocha anayekomesha nidhamu mbovu kwenye kikosi huku wengine wakiwa tofauti wakisema anakosea kuwatukana wachezaji na kuwagombeza kama watoto wadogo jambo ambalo sio sawa.

Lakini pia wengine wakawa wanamlalamikia kwa kitendo cha kumuingiza na kumtoa baada ya dakika 12 mshambuliaji Betram Mwombeki aliyechukua nafasi ya Hamis Tambwe na yeye nafasi yake ikachukuliwa na Henry Joseph Shindika.

UONGOZI
Uongozi wa Simba chini ya mwenyekiti wake Ismail Aden Rage unaendelea kushughulikia mzozo huo wa Owino na Loga ili kupata utatuzi wa kuinufaisha timu hiyo kwa mzunguko wa pili wa ligi kuu ambao bado Simba wapo kwenye nafasi ya nne.

FA CUP : Man City vs Chelsea,Arsenal vs Liverpool watauana

Manchester City ya Manuel Pellegrin watacheza dhidi ya Chelsea ya Jose Mourinho, wakati Arsenal watakuwa nyumbani kuwaalika Liverpool kwenye michezo ya raundi ya tano ya kombe la FA.

Boss wa Everton Roberto Martinez atacheza dhidi ya moja ya timu alizowahi kufundisha Swansea,huku Sunderland ikipangwa kukipiga na Southampton.

Ratiba kamili

Manchester City v Chelsea
Sheffield United or Fulham v Nottingham Forest or Preston North End
Arsenal v Liverpool
Brighton & Hove Albion v Hull City
Cardiff City v Wigan Athletic
Sheffield Wednesday v Charlton Athletic
Sunderland v Southampton
Everton v Swansea City

Friday, January 17, 2014

Wasomali kuichezesha Yanga

Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka Somalia kuchezesha mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Yanga ya Tanzania na Komorozine Sports ya Comoro.

Mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya mchujo itafanyika jijini Dar es Salaam kati ya Februari 7 na 9 mwaka huu wakati ile ya marudiano itachezwa kisiwani Comoro kati ya Februari 14 na 16 mwaka huu.

Mwamuzi wa kati atakuwa Hassan Mohamed Hagi wakati wasaidizi wake ni Hamza Hagi Abdi, Bashir Abdi Suleiman na Bashir Olab Arab. Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Eugene Musoke kutoka Uganda.

Timu ambazo zimeingia moja kwa moja katika raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa ni Coton Sport ya Cameroon, El Ahly (Misri), TP Mazembe (Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), El Hilal (Sudan), Club Sportif Sfaxien (Tunisia) na Esperance (Tunisia)

Nayo mechi ya kwanza ya raundi ya mchujo kati ya Azam ya Tanzania na Ferroviario Da Beira ya Msumbiji itakayofanyika Dar es Salaam kati ya Februari 7 na 9 mwaka huu itachezeshwa na waamuzi kutoka Sudan.

Waamuzi hao ni Mutaz Abdelbasit Khairalla atakayepuliza filimbi, Waleed Ahmed Ali, Aarif Hasab Elton na El Fatih Wadeed Khaleel. Kamishna wa mechi hiyo ni Hassan Mohamed Mohamed kutoka Somalia. Mechi ya marudiano itachezwa Msumbiji kati ya Februari 14 na 16 mwaka huu.

Timu zilizotinga moja kwa moja katika raundi ya kwanza ya michuano hiyo ni Asec Mimosas ya Ivory Coast, Ismailia (Misri), Wadi Degla (Misri), Djoliba (Mali), MAS (Morocco), Bayelsa United (Nigeria), El Ahly Shandy (Sudan), E.S.S. (Tunisia), C.A.B. (Tunisia) na Zesco United (Zambia).