Tuesday, August 27, 2013

Bale aipasua kichwa Spurs



Mshambuliaji wa Tottenham Gareth Bale ameshindwa kutokea kwenye mazoezi ya timu hiyo aliyotakiwa kuripoti leo akitokea Marbella.

Bale, 24,anatajwa kuwa karibu kuweka rekodi ya dunia ya dau la paundi milioni 86 kutoka kwa Real Madrid lakini Spurs wamesema hakuna makubaliano yaliyofikiwa.
 
Tottenham imepokea offer nyingine nje ya Real Madrid japo bado haijatajwa lakini inaelezwa kuwa ni Manchester United.

Spurs walimtaka Bale kuripoti leo Jumanne lakini hakuna sababu zozote zilizotolewa za kushindwa kutokea.
Inaaminika kuwa huko Hispania Real Madrid wametengena stage iliyopewa jina la 'Bale Box', ambayo imewekwa kwenye uwanja wao wa Santiago Bernabeu itakayotumika kumtambulisha kwa mashabiki wa klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.