Friday, August 30, 2013

Etoó ndani ya Chelsea,Mourinho meno yote nje,Torres awekwa sokoni

Kutua kwa mshambuliaji Samuel Etoó Fils kutakuwa kumeshusha presha ya kocha wa Chelsea Jose Mourinho The Happy One.

Mourinho alikuwa anasaka mshambuliaji baada ya kutofurahia kazi ya upachikaji mabao inayofanywa na Fernando Torres,Demba Ba na Romelu Lukaku ambao sasa inabidi wakaze mkwiji kama wanataka kuendelea kungára kwenye timu hiyo.
Baada ya kutua kwa mshambuliaji huyo raia wa Cameroon sasa Fernando Torres amewekwa sokoni na Chelsea wako tayari kusikiliza ofa.

Torres amekuwa hana uhakika wa namba tokea alipotua kwenye klabu hiyo kwa dau la paundi milioni 50 lililoweka rekodi ya uhamisho England akitokea Liverpool.
 Licha ya Demba Ba kutakiwa na Newcastle United Mourinho hana uwoga wa kumuuza Torres kwakuwa anaamini Lukaku atakuwa msaada mkubwa kwa timu hiyo na yumo kwenye mipango yake.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.