Thursday, August 8, 2013

Chelsea ya Mourinho yavikwa ubingwa England,Man U yatupwa,Arsenal Spurs watauana

Programme mpya ya computer imetabiri kuwa kikosi cha Chelsea chini ya kocha Jose Mourinho ndio watavikwa taji la ligi kuu ya England itakapofika mwisho wa msimu.

Mahesabu hayo pia yanaonesha kuwa Tottenham,wakiwa na Gareth Bale au wakiwa bila ya mshambuliaji huyo watapambana kwa mara nyingine na Arsenal katika vita ya kuwania nafasi ya nne kucheza ligi ya mabingwa Ulaya.

Programme hiyo ya Computer inaonesha kuwa kutua Chelsea kwa Marco van Ginkel, Andre Schurrle na Mark Schwarzer kutawabeba na kuwaimarisha watoto hao wa darajani kiasi cha kukaa juu ya mahasimu wa mji mmoja Manchester United na Manchester City.
Timu ya Manchester City chini ya Manuel Pellegrini wanaonekana kuwa watamaliza nafasi ya pili juu ya mahasimu wao Manchester United.
 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.