Monday, September 30, 2013

Yanga yaibuka na mpango wa kujenga Jangwani City

 
Klabu ya Yanga sasa imeibuka na mpango wa kujenga mji wake eneo la Jangwani utakaoitwa Jangwani City.

Mwenyekiti wa bodi ya wadhamini wa klabu hiyo Francis Kifukwe amesema tayari wameomba kuongezwa eneo la ziada ili kujenga mji huo wa kisasa.

Kifukwe amesema mji huo wa Jangwani utakuwa na viwanja mbalimbali vya mazoezi pamoja na uwanja mkubwa utakaobeba watu elfu 40 pamoja na viwanja vingine vidogo vidogo vya mazoezi na vya timu za watoto.

Aidha mji huo utakuwa na maduka mbalimbali ya kufanya shopping,kumbi za starehe na kumbi za mikutano.

Tayari klabu hiyo imepeleka maombi wizara ya ardhi,nyumba na maendeleo ya makazi ili waweze kuongezewa eneo la kufanya hivyo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.