Friday, September 27, 2013

Hizi ndio busara za Balotelli


Mshambuliaji wa AC Milan Mario Balotelli ameomba radhi kwa wachezaji wenzake na mashabiki kwa kadi nyekundu aliyopewa Jumamosi kwenye mchezo wa ligi kuu ya Italia Serie A uliokwisha kwa timu hiyo kuchapwa mabao 2-1 na Napoli.

Mshambuliaji huyo alioneshwa kadi hiyo baada ya kutoa maneno makali kwa mwamuzi Luca Banti na amekumbana na adhabu ya kufungiwa mechi tatu.

Balotelli amesema anaomba radhi kwa wachezaji wenzake kwakuwa kitendo alichokifanya hakiisaidi timu hiyo huku pia akijutia kwa kusema anajihisi ni mkosaji mbele ya mashabiki wanaoijali timu.

Amesema amefanya kosa kwa kutoa maneno makali dhidi ya mwamuzi lakini anasema hataomba radhi kwa kila mmoja isiwe kama ameua mtu.

Baada ya kupewa kadi klabu ya AC Millan iliamua kutokata rufaa kupinga maamuzi ya kufungiwa kwa mshambuliaji huyo na kocha Massimiliano Allegri akasema Balotelli ana miaka 23 sio motto,amefanya kosa linaighalimu timu na mashabiki,inampasa abadili muenendo wake wa tabia.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.