Wednesday, September 25, 2013

Ashanti United,Rhino patachimbika Tabora leo

Leo katika ligi kuu soka Tanzania bara kunapigwa mchezo mmoja tu kwenye uwanja wa Ally Hassan Mwinyi Tabora wakati Ashanti United itakaposhuka dimbani kukipiga na Rhino Rangers.

Timu hizo zote mbili zimepanda daraja msimu huu na zinajua msoto wa ligi daraja la kwanza ili kupanda ligi kuu.

Ashanti angalau walishawahi kuinusa ligi kuu hapo kabla tofauti na Rhino Rangers ambao ni mara yao ya kwanza kuonja utamu wa ligi kuu hivyo hawatakuwa tayari kuukosa kwa kurudi walipotoka huku Ashanti nao wakikumbuka msoto wa kurudi ligi kuu hawatapenda kupoteza nafasi katika wakati ambao wanasota mkiani mwa msimamo wa ligi.

Wauza mitumba hao wa Ilala Ashanti wana pointi moja tu mpaka sasa baada ya kupata sare ya bao 1-1 mbele ya Azam FC lakini imekubali kichapo katika michezo yake yote mingine iliyocheza.

Imechapwa na Yanga 5-1,imefungwa na JKT Ruvu na Mgambo JKT bao 1-0 kila mmoja huku pia ikichapwa na Kagera Sugar katika mchezo uliopita kwa mabao 3-0 kwenye dimba la Kaitaba.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.