Monday, September 30, 2013

Mancini mguu sawa Galatasaray

Bosi wa zamani wa Manchester City Roberto Mancini yupo karibu kutua Galatasaray na sasa wapo katika mazungumzo.

Galatasaray,ambayo ilimtimua kocha Fatih Terim wiki iliyopita imethibitisha kwenye mtandano wake wa Twitter kuwa inakutana na kocha huyo MTaliano mwenye miaka 48 huko Istanbul.

Rais wa klabu hiyo Unal Aysal na mtendaji mkuu Lutfi Aribogan wamekutana na Mancini,na klabu hiyo imetuma picha zinazowaonyesha watatu hao wakiwa pamoja.

Mancini alitimuliwa na Manchester City mwezi May ikiwa ni mwaka mmoja tokea ameiongoza klabu hiyo kutwaa taji la ligi kuu ya England huku pia akiiongoza klabu hiyo kutwaa taji la FA.

Timu hiyo ipo kwenye nafasi ya 10 ikiwa na pointi saba ambazo ni pointi 8 nyuma ya vinara wa ligi hiyo Fenerbache.
Itakumbukwa pia katika Champions league walikutana na kisago cha mabao 6-1 kutoka kwa Real Madrid katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.