Monday, September 30, 2013

Wenger aichokonoa Chelsea,amjaza upepo Benitez

 
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amesema kocha Rafael Benitez alipewa wakati mgumu amkiwa Chelsea lakini anaamini historia itaonesha kuwa aliwafanyia kazi nzuri.

Benitez, 53, atatua na kikosi chake cha Napoli huko London kesho kukipiga na the Gunners katika mchezo wa Champions League.

Kocha huyo alipewa kibarua cha muda kuinoa Chelsea November mwaka uliopita akiiongoza kuchukua taji la Europa league lakini hakukubalika kwa mashabiki wa klabu hiyo.

Wenger anasema Benitez hakutendewa vizuri kwakuwa hawakutarajia kuwa iko siku angeifundisha klabu hiyo lakini alifanya vizuri na muda unavyozidi kwenda watakuja kukubali alichokifanya.
 

Benitez,ambaye aliiongoza Chelsea kumaliza nafasi ya tatu katika ligi kuu,aliondoka Stamford Bridge na kukabidhiwa mikoba ya kukinoa kikosi cha Napoli kuanzia mwezi May na hapo kesho ataiongoza klabu hiyo ya Serie A kwenye mchezo wa kundi F dhidi ya Arsenal.

Timu zote zinakutana zikiwa zimeshinda mechi zake za kwanza za kundi hilo linaloongozwa na Arsenal lakini hata katika ligi Napoli wapo nafasi ya pili wakati Arsenal wanaongoza ligi.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.