Friday, September 27, 2013

Tunisia Majanga,Fifa yatishia kushusha rungu


Waziri wa michezo wa Tunisia Tarek Dhiab ametakiwa kuweka mambo sawa kwenye shirikisho la soka la nchi hiyo,FIFA wakionya kuwa serikali kuvuka mipaka yake na kuingia kwenye masuala ya shirikisho hilo ni kitendo kinachotafsiriwa kama serikali kuingilia masuala ya soka.

Dhiab amewashtua wapenda michezo wan chi hiyo ya Africa kaskazini baada ya kuwataka FIFA kulivunja shirikisho la soka la nchi hiyo bila ya kuwepo kwa sababu zozote.

Fifa wamepingana na hilo na kuitaka serikali kukaa mbali na shirikisho la soka au watachukulia ni kitendo cha serikali kuinvilia masuala ya mpira ambayo adhabu yake ni kufungiwa kujihusisha na soka.

Waziri mkuu wa Tunisia Ali Laarayedh ameitisha haraka mkutano wa kuweka sawa mambo ambao utahudhuriwa na wajumbe wa chama cha soka na wawakilishi wa Waziri wa michezo.

Klabu za Tunisi zinashiriki kwenye ligi ya mabingwa na kombe la shirikisho wakati timu ya Taifa itacheza na Cameroon kwenye mchezo wa kuisaka tiketi ya fainali za kombe la dunia 2014.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.