Tuesday, September 24, 2013

Andy Murray afanikiwa oparesheni ya mgongo


Mcheza Tennis namba moja Uingereza Andy Murray ametuma picha yake kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter akionesha vidole gumba vyake katika ishara ya kwamba yuko sawa baada ya kufanyiwa oparesheni ndogo ya mgongo.

Murray mwenye miaka 26 anatarajia kuanza mazoezi yake ya kabla ya msimu huko Miami mwezi November.

Maumivu hayo aliyofanyiwa oparesheni yalisababisha kutangaza kujiondoa kwenye mashindano ya wazi ya Ufaransa mwezi May lakini akafanikiwa kurejea kwenye michuano ya Wimbledon aliyofanikiwa kushinda na kuwa mchezaji wa kwanza wa kiume kushinda taji hilo tokea mwaka 1936.

Utetezi wake wa US Open iliishia hatua ya robo fainali lakini aliisaidia Great Britain kuifunga Croatia kwenye Davis Cup kabla ya kufanyiwa oparesheni hiyo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.