Thursday, September 19, 2013

TFF yatoa siku 14 kwa klabu kupeleka mikataba ya makocha

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF limetoa siku 14 kwa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom na za Ligi ya Daraja la Kwanza kuwasilisha mikataba ya makocha wao.

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF iliyokutana Septemba 12 mwaka huu imebaini klabu nyingi hazijawasilisha mikataba ya mabenchi yao ya ufundi, kitu ambacho ni matakwa ya kikanuni.

Siku hizo 14 zimetolewa kuanzia Septemba 17 mwaka huu.

Kwa klabu ambazo zitashindwa kuwasilisha mikataba hiyo na vielelezo vingine ndani ya mudau huo zitachukuliwa hatua kwa mujibu wa kanuni.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.