Friday, September 27, 2013

Ngassa aonesha jeuri ya pesa,alipa deni la Simba,asema aliyeguswa anaweza kumchangia

Kiungo mshambuliaji wa timu ya Yanga Mrisho Ngassa leo amelipa jumla ya milioni 45,ikiwa ni fedha ya deni la shilingi milioni 30 pamoja na faini ya milioni 15 za klabu ya Simba kwa Shirikisho la Soka nchini TFF ili aweze kuitumikia timu yake kuanzia kesho.

Ngassa ambaye aliambatana na viongozi wa klabu ya Yanga mjumbe wa sekretarieti Partick Naggi, Afisa Habari Baraka Kizuguto na mhasibu Rose Msamila alikabidhi hundi za malipo kwa idara ya fedha ya shirikisho hilo.

Mara baada ya kukabidhi hundi hiyo Ngassa aliongea na waandishi wa habari nje ya ofisi za TFF na kusema ameamua kulilipa deni hilo ili aweze kuitumikia klabu yake, kwakuwa kukosa michezo sita kumemnyima nafasi kuisaidia timu yake.

Ngassa amesema anaomba aeleweke kuwa fedha hizo amezitoa mwenyewe kwenye akaunti yake ya benki na kuwataka wale wote walioguswa na suala hilo wanaweza kumchangia.

Amesema sasa akili yake yote ipo kwenye Ligi Kuu na lengo lake ni kuhakikisha anaisadia timu yake kufanya vizuri na kupata ushindi katika kila mchezo watakaocheza.

Kocha Ernie Brandts kwa sasa ana fursa ya kumtumia mchezaji huyo kwa kuanzia na mchezo wa kesho baada ya kukamilisha adhabu yake aliyopewa ya kukaa nje kwa mechi sita na akulipa kitita cha shilingi milioni 45.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.