Thursday, September 26, 2013

Arsenal,Chelsea uso kwa uso Capital One

Arsenal watakuwa wenyeji wa Chelsea katika mchezo wa raundi ya nne ya michuano ya Capital One.


Arsenal wametinga hatua hiyo baada ya kuwasukuma nje West Bromwich Albion kwa njia ya matuta hapo jana wakati Chelsea walikata tiketi baada ya kuwachapa Swindon Town kwa maboa 2-0 Jumanne.

Manchester United baada ya kuwasukuma nje Liverpool hapo jana sasa watakutana na Norwich City,wakati Manchester City watakuitana na Newcastle.

Mechi hizo zinatarajia kupigwa October 28.

Draw imeamua mechi hizi.
Sunderland v Southampton
Leicester City (II) v Fulham
Birmingham City (II) v Stoke City
Manchester United v Norwich City
Burnley (II) v West Ham United
Arsenal v Chelsea
Tottenham Hotspur v Hull City
Newcastle United v Manchester City

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.