Thursday, September 26, 2013

Kocha Banyai akana kuikacha Ashanti


Kocha mkuu wa Ashanti United Hassan Banyai amekana kuikacha timu hiyo.

Banyai amesema ameomba ruhusa ya kushughulikia matatizo yake ya kifamilia na ataungana na timu hiyo baada ya mchezo wake na Mtibwa Sugar.

Amesema kumekuwa na maneno mengi yasiyo na ukweli lakini ukweli uko wazi na hata uongozi unafahamu kila kitu kuhusu matatizo yake ya kifamilia na ndio maana aliomba ruhusa na ikakubaliwa.

"Kaka mimi bado ni kocha wa Ashanti,lakini nilipata matatizo ya kifamilia ndio nayashughulikia,kama huamini muulize Mgoyi(Msafiri)Rais wa Ashanti au waulize viongozi wengine watakwambia ukweli kuwa sijaacha wala sijafukuzwa"alisema Banyai.
Kumekuwa na maneno maneno kuwa kocha huyo ameikimbia timu hiyo baada ya kuwa na mwendendo mbovu katika ligi mpaka sasa ikiwa imefungwa mechi tano na kutoka sare mchezo mmoja.

Hata hivyo Banyai amewataka mashabiki kutulia kwakuwa atarejea katika kikosi hicho baada ya mechi dhidi ya Mtibwa Sugar.

Ashanti jana ilichukua kipigo kingine katika ligi,ikikubali kuchapwa mabao 2-0 mbele ya Rhino Rangers ya Tabora kwenye uwanja wa Ally Hassan Mwinyi.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.