Tuesday, September 24, 2013

PUMA wamtia kitanzi Usain Bolt


Bingwa wa michuano ya Olympic mkwanariadha Usain Bolt ameongeza mkataba wake na kampuni ya vifaa vya michezo ya Ujerumani PUMA mpaka mwaka 2016 baada ya mashindano yatakayofanyika huko Rio de Janeiro.

Bolt raia wa Jamaica mwenye miaka 27,amekuwa na mkataba na Puma tokea mwaka 2003,na mwanariadha huyo amesema anajivunia kuongeza mkataba na Puma kwa miaka kadhaa.

Mapema alisema kuwa anataka kustaafu mchezo huo baada ya mashindano ya mwaka 2016 lakini sasa amesema anaweza kushindana kwa mwaka mmoja zaidi.

Bolt ameshinda medali sita za dhahabu za Olympic na nane za mashindano ya dunia na rekodi yake yam kukimbia kwa sekunde 9.58 katika mbio za mita 100 inaendelea kusimama mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.