Friday, September 27, 2013

Villas Boas asema hana urafiki na Mourinho,yeye apindua stori


Kocha wa Tottenham Andre Villas-Boas hajali lolote kuhusu kuvunjika kwa mahusiano yake na boss wake wa zamani ambaye sasa anafundisha Chelsea, Jose Mourinho.

Villas-Boas, 35, alifanya kazi chini ya Mourinho kwa miaka saba wakiwa FC Porto, Chelsea na baadaye Inter Milan na anakutana naye kwa mara ya kwanza wakati the Blues itakapokwenda White Hart Lane kesho.
Kocha huyo anasema alikuwa rafiki wa Mourinho wakati huo,urafiki ambao haupo wakati huu.

Hata hivyo Mourinho kwa upande wake hakutaka kuzungumza lolote kuhusu mahusiano yao na AVB akisema hana la kusema lakini akapindua stori akiwaweka Spurs kuwa moja ya timu zinazowania ubingwa.
Amesema mbio za ubingwa sasa zipo kwa timu sita tofauti na miaka ya nyuma mbio hizo ilikuwa kwa timu mbili.

Mourinho anasema wakati akiifundisha Chelsea kwa mara ya kwanza alikuwa anafukuzia ubingwa na Manchester United peke yake lakini sasa mambo yamebadilika kuna timu zipatazo sita wakiwemo Spurs wanaocheza nao kesho.
Timu sita zinazotajwa ni Chelsea,Manchester United,Manchester City,Arsenal,Liverpool na Spurs.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.