Wednesday, July 31, 2013

Simba yasajili kifaa kingine

Wekundu wa Msimbazi Simba leo wamekamilisha usajili wa mshambuliaji Betram Mwombeki aliyekuwa anasoma Marekani.

Mshambuliaji huyo alikuwa kwenye majaribio kwa wekundu hao ambao amefaulu na kupewa mkataba wa miaka miwili ya kuitumikia timu hiyo na ameusaini mbele ya kaimu makamu mwenyekiti Joseph Itangáre Kinesi.

Mwombeki mwenye mwili mkubwa anakumbukwa kwa kutupia bao kwenye mchezo wa kirafiki ambao wekundu hao wa Msimbazi walicheza dhidi ya URA kwenye uwanja wa Taifa Dar Es Salaam.

Simba wanaendelea kuimarisha kikosi chao na safu ya ushambuliaji ikiwa tayari pia imemsajili mshambuliaji kutoka Burundi Hamissi Tambwe.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.