Monday, July 29, 2013

Bayern Munich kuvunja benki kumnasa Luiz

 

Bayern Munich iko tayari kutoa ofa ya paundi milioni 40 ili kumnasa beki wa Chelsea David Luiz.

Bosi wa Bayern Pep Guardiola alikuwa akihitaji huduma ya beki huyo tokea alipokuwa akiifundisha Barcelona na sasa akiwa kwa mabingwa wa Ulaya yuko tayari kuingia kwenye mbio za kumnasa.

Beki huyo aliyekuwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Brazil kilichotwaa ubingwa wa Confederation amerejea kujiunga na Chelsea kwenye maandalizi ya kabla ya msimu akiwa chini ya kocha mpya Jose Mourinho na Guardiola anarejea kwenye mbio za kumsajili.


Bayern wamekula kibano cha mabao 4-2 kutoka kwa mahasimu wao Borussia Dortmund kwenye German Super Cup Jumamosi na wanaona bado wanahitaji kuimarisha kikosi.

Inaaminika kuwa Bayern wako tayari kupanda dau mpaka kufikia paundi milioni 45 pamoja na bonasi kitu ambacho ni faida kubwa kwa Chelsea kama wakikubali kwakuwa beki huyo walimnasa kwa dau la paundi milioni 21 kutoka Benfica miaka miwili iliyopita.

Wakati huo huo wachezaji wawili wa zamani wa Chelsea Florent Malouda na Jose Bosingwa leo wanakamilisha kujiunga na Trabzonspor ya Uturuki.

Malouda, 33,aliruhusiwa na Blues kuondoka mwishoni mwa msimu uliopita wakati Bosingwa, 30 hakuwa na furaha kwenye kikosi cha QPR alichojiunga nacho akitokea Chelsea.

Ana show lov kwa klabu mpya


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.