Friday, July 26, 2013

Utata wa umri wa Falcao wamalizwa,cheti cha kuzaliwa hadharani

Ubishi wa utata wa umri wa mshambuliaji nyota wa Colombia Radamel Falcao umemalizwa baada ya gazeti moja la Colombia kukiweka hadharani cheti za kuzaliwa cha nyota huyo.

Utata wa umri wake ulikuja baada ya mwalimu mkuu wa zamani wa mshambuliaji huyo kuzungumza kwenye televisheni ya Colombia Noticias Uno akisema Falcao amezaliwa 1984 na sio 1986.

Lakini gazeti la El Tiempo limechapisha cheti za kuzaliwa kutoka manispaa ya Santa Marta kinachoonesha kuwa mshambuliaji huyo kazaliwa February 10, 1986,na hivyo sasa ana umri wa miaka 27 na sio 29.


Nyaraka inayodai Falcao alizaliwa 1984, sio 1986 

Nyaraka kutoka shule ya msingi aliyosoma Falcao
Hii ndio inayothibitisha umri sahihi wa Falcao ikionesha kazaliwa 1986
 Hapa jembe likitambulishwa Monaco
 Jembe kazini na jezi za Monaco
Falcao alitua Monaco ya Ufaransa akitokea Atletico Madrid ya Hispania kwa dau la paundi milioni 53 na kumfanya kuwa mchezaji ghali zaidi kusajiliwa kwenye ligi ya Ufaransa kabla ya Ednson Cavani kuweka rekodi mpya baada ya kusajiliwa na PSG kwa dau la paundi milioni 55.

1 comment:

Note: Only a member of this blog may post a comment.