Wednesday, July 31, 2013

Madrid watumbukia rasmi na gia kubwa kwa Bale

Real Madrid wametumbukia rasmi na kuweka dau linaloweka rekodi ya dunia katika uhamisho wa wachezaji baada ya kuweka mezani paundi milioni 85 ili kumnasa mshambuliaji wa Tottenham Gareth Bale.

Dau la Real Madrid linaelezwa kuwa lipo mezani kwa karibia wiki sasa ambalo linamchanganya Bale aliyeomba kutaka kuzungumza na wakali hao wa Hispania.
Dau hilo lililowekwa mezani halihusishi mchezaji yeyote wa Real madrid kutolewa kwenda Spurs kama sehemu ya mpango huo.
Tottenham na Bale wamerudi kutoka kwenye Asia Trophy na leo wanarudi mazoezini kujiandaa na msimu mpya wa EPL.

Mchambuzi wa Sky Sports mchezaji wa zamani wa Spurs Jamie Redknapp anasema anafikiri sasa ni wakati wa Bale kuondoka.


Anasema unawezaje kukataa dau kubwa kama hilo huku akiamini klabu hiyo haiwezi kukataa kuuza kwasababu ni kawaida yake akitolea mfano wa Michael Carrick, Luka Modric, na Dimitar Berbatov.
 

Mchezaji ambaye anakamata rekodi ya dunia mpaka sasa ni Cristiano Ronaldo ambaye alitua Madrid mwaka 2009 kwa dau la paundi milioni 80.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.