Friday, July 26, 2013

Bunduki za Starz kuiua Uganda hizi hapa

Kocha wa timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Starz iliyopo Kampala nchini Uganda kwa mchezo wa kuisaka tiketi ya fainali za mataifa bingwa barani Africa CHAN dhidi ya wenyeji Uganda The Cranes,Kim Paulsen ametaja silaha zake zitakazoanza kesho kuusaka ushindi.

Kim ameamua kumuanzisha kiungo Athuman Idd Chuji ambaye kwenye mchezo wa kwanza uliopigwa uwanja wa Taifa na Starz kulala kwa kufungwa bao 1-0,Chuji alikula benchi na huenda kukosekana kwa kiungo Mwinyi Kazimoto aliyetoroka kambini ikawa imefungua njia ya yeye kuanza.

Stars inatarajiwa kupangwa hivi; Juma Kaseja, Erasto Nyoni, David Luhende, Aggrey Morris, Kelvin Yondani, Athuman Idd, Salum Abubakar, Frank Domayo, John Bocco, Amri Kiemba na Mrisho Ngasa

Moja ya mikakati ya Taifa Stars kwenye mechi hiyo ya keshokushambulia kwa muda mwingi wa mchezo.

Kim amesema maandalizi ya Taifa Stars jijini Mwanza kwa ajili ya mechi hiyo ambayo Uganda inaongoza kwa bao 1-0 yalikuwa mazuri, lakini mabao ni muhimu hivyo watashambulia bila kusahau kulinda lango lao.

Amesema katika mechi ya kwanza walitengeneza nafasi nyingi lakini hawakuzitumia, hivyo wamekuwa wakifanya mazoezi ya kushambulia, jinsi ya kutengeneza nafasi, na jinsi ya kumalizia.

Amesema angalau kutakuwa na mabadiliko kwa kuingiza sura mbili mpya katika kikosi cha kwanza, na kuongeza kuwa wachezaji wanafahamu umuhimu wa mechi hiyo kwani timu ikienda kwenye Fainali za CHAN itakuwa manufaa kwao binafsi.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imefanya mazoezi ya mwisho leo jioni Uwanja wa Mandela ulioko Namboole ambao utatumika kwa ajili ya mechi hiyo kesho.

Mechi hiyo itaanza saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki na itachezeshwa na waamuzi kutoka Madagascar wakiongozwa na Kanoso Abdoul Ohabee wakati mwamuzi msaidizi namba moja ni Andirvoavonjy Pierre Jean Eric. Mwamuzi msaidizi namba mbili ni Jinoro Velomanana Ferdinand huku Andriamiharisoa Hubert Marie Bruno akiwa mwamuzi wa mezani (fourth official). Kamishna wa mechi hiyo namba 38 ni Ismail Kamal kutoka Ethiopia.

Kutoka kwa Supermariotz : MUNGU IBARIKI TANZANIA,MUNGU IBARIKI TAIFA  STARZ

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.