Wednesday, July 17, 2013

CHOKOCHOKO : Chelsea watumbukiza rasmi ofa kwa Rooney,United yakomaa


Mashetani wekundu wa Manchester United wameikataa ofa ya Chelsea ya kutaka kumnasa mshambuliaji Wayne Rooney na wamesisitiza hauzwi.

Chelsea wamethibitisha kupeleka ofa ya United lakini wamekanusha kuwa walipeleka ofa ya fedha pamoja na kutaka kumtoa mmoja kati ya kiungo mchezeshaji Juan Mata au beki David Luiz.

Rooney amechukukizwa na kuchanganywa na nafasi yake ndani ya kikosi hicho cha United baada ya bosi mpya David Moyes kuweka wazi kuwa mshambuliaji huyo hatakuwa chaguo lake la kwanza Old Trafford.
Rooney, 27,ameelezea hisia zake za kukatishwa tamaa na amesema hatakubaliana na mtindo wa kucheza kwa mzunguko tena akiwa chaguo la pili nyuma ya Mholanzi Robin van Persie na hiyo ikawa sababu ya Chelsea kutumbukiza ofa ya kutaka kumnasa.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.