Sunday, July 28, 2013

BREAKING NEWS : Yanga yapinga Azam Media kuonesha ligi kuu

Kamati ya utendaji ya klabu ya Yanga inakutana muda huu ajenda kubwa ikiwa kupinga Azam Media kupewa haki za kuonesha mechi za ligi kuu soka Tanzania bara msimu ujao.

Kwa mujibu wa mmoja w wajumbe wa kamati hiyo ya utendaji anasema kikubwa wanachotaka kupinga ni kutotangazwa kwa tenda ili washindani wengi zaidi wajitokeze kuwania nafasi hiyo.

Anasema kingine wanachopigania ni kutaka kulipwa fedha zaidi ya vilabu vingine kwakuwa wanaamini wao ni timu kubwa ambayo inaingiza mashabiki wengi zaidi kuliko timu nyingine ambazi hazina mtaji wa mkubwa wa mashabiki.

Hata hivyo kwa mujibu wa sheria ya FIFA haki za kuoneshwa kwa ligi ya nchi husika inamalikiwa na chama cha soka ama shirikisho la nchi hiyo.

Ijumaa Azam Media na kamati ya ligi walitangaza kufikia muafaka wa kusaini mkataba wa miaka mitatu kwa kampuni hiyo ya habari kuonesha mechi za ligi kuu.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.