Tuesday, July 30, 2013

Lewandowski haendi kokote


Mshambuliaji wa Borussia Dortmund Robert Lewandowski ameahidi kuendelea kucheza Borusia Dortmund kwa moyo wote licha ya kushindikana kuhamia Bayern Munich.

Lewandowski, ambaye mkataba wake na Dortmund unamalizika mwakani amekataa kuongeza mkataba mpya msimu uliopita akisema angejiunga na klabu ya chaguo lake.


Baada ya sakata la mwezi mzima la uhamisho wake na kikaribia kuwa mchezaji wa pili wa Dortmund kunaswa na mahasimu wao Bayern baada ya kufanya hivyo kwa Mario Goetze, Dortmund wakazuia mpango huo.
Mshambuliaji huyo mwenye miaka 24 hajaonesha kuchukizwa na kitendo hicho cha kuzuiwa kuondoka huku akiichezea timu hiyo kwenye mchezo wa German Cup Jumamosi.
 
Lewandowski tayari ana taji la kwanza la msimu baada ya Dortmund kuichapa Bayern kwa mabao 4-2 Jumamosi iliyopita kwenye German Cup.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.