Saturday, July 13, 2013

Tambwe atuliza mzuka Simba



Mshambuliaji mpya aliyesajiliwa na Wekundu wa Msimbazi Simba Amissi Tambwe ndio imekuwa gumzo la usajili kwa wekundu hao baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili hapo jana.

Tambwe ametua akitokea Vital’O,ya Burundi na ametupia wavuni mabao 18 kwenye msimu uliopita na kunyakuwa kiatu cha dhahabu kwenye ligi ya Burundi.

Mshambuliaji huyo ameibuka pia mfungaji bora wa michuano ya klabu bingwa Africa mashariki na kati maarufu kombe la Kagame,michuano iliyomalizika huko Sudan kwa Vital'o kuibuka na ubingwa.
         Karibu Tanzania mimi ndio Zakharia Hanspope

Tambwe ambaye ndiye mshambuliaji chaguo la kwanza kwenye timu ya Taifa ya Burundi Inthamba Murugamba amekuwa mchezaji wa nne raia wa kigeni kwa msimu huu kutua Simba huku wengine wakiwa bado wanasotea kusajiliwa wakiwemo Mganda Assumani Buyinza,Samuel Ssenkoomi, MCongo Felix Cuipo na James Kun kutoka Sudan Kusini.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.