Wednesday, July 31, 2013

JEURI YA PESA : Spurs wataka kuifanyia umafia Arsenal,wafikiria kutumbukiza mkono kwa Suarez


Wakati wa usajili kuna wengine huwa wanaachwa na maumivu na kuna wengine huwa wanamaliza kipindi hicho wakiwa wanacheka meno yote nje.

Sasa habari mbaya kwa Arsenal ni kwamba Tottenham wanaweza kuwafanyia umafia mahasimu wao hao wa London Kaskazini na kumchukua Luis Suarez kutoka Liverpool,kama Gareth Bale atakamilisha taratibu za kutua Real Madrid.
 
Tayari Madrid wameweka mezani paundi milioni 85 za kumtaka Bale japo mwenyekiti wa Spurs Daniel Levy anaweka ngumu anataka paundi milioni 126.

Habari hizo zinaweza kuwa si nzuri kwa mashabiki wa Arsenal ambao wanaamini Suarez ataisaidia timu hiyo japo Liverpool bado wameweka ngumu kumuuza kwa dau la chini ya paundi milioni 50.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.