Wednesday, July 31, 2013

Valencia yamchokonoa Torres

 
Fernando Torres amepewa ofa ya kuondoka Chelsea na kutua Valencia ya Hispania kwa dau la paundi milioni 20.

Valencia wanataka kutumbukia kwa Torres wakiamini kuwa anaweza kuwa mbadala wa Roberto Soldado anayetakiwa na Spurs.

Bosi wa Valencia Miroslav Duckic alijaribu kutaka kumnasa mshambuliaji wa Arsenal Olivier Giroud, huku pia mshambuliaji wa Real Zaragoza Mreno Helder Postiga akiwa ndiye mshambuliaji anayewezekana kutua kwenye timu hiyo kwasasa.
 
Kukiwa na uwezekano wa kutua kwa mshambuliaji Wayne Rooney kutokea Manchester United inaonekana itampa wakati mgumu Torres ya kupata nafasi kwenye kikosi cha kwanza.

Torres tokea ametua Chelsea kwa dau la paundi milioni 50 mwaka 2011 bado hajaonesha cheche zake akifunga mabao nane kwenye mechi 28 za EPL alizocheza na akitupia jumla ya mabao 23 kwenye mashindano yote akiwa na The Blues.


Ameibuka mfungaji bora kwenye Confederations Cup akiwa na kikosi cha Hispania chini ya Vicente del Bosque.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.