Monday, July 29, 2013

Yanga yaipinga rasmi bodi ya ligi TPL kuipa haki Azam Media kuonesha mechi za ligi kuu

 Mabingwa wa Tanzania Yanga Africa wametangaza rasmi kupinga mechi za ligi kuu soka Tanzania bara kuoneshwa na Azam Media kupitia kituo chake cha televisheni Azam Tv baada ya kupata haki ya kuonesha mechi hizo wakikishinda kituo cha televisheni cha nchini Africa kusini cha Superspot.

Kikao cha kamati ya utendaji cha klabu hiyo kilichoketi jana kimeamua kupinga hatua hiyo ya Azam media kupewa haki hizo za televisheni na bodi ya ligi kuonesha ligi kuu kwa miaka mitatu kutokea msimu ujao utakaoanza kuunguruma August 24.

Mwenyekiti wa Yanga Yusuph Mehboob Manji amesema mkataba huo hauko wazi wenye mgongano wa kimaslahi,kwakuwa kampuni hiyo ndio inayoimiliki Azam FC ambao ni maadui wakubwa wa Yanga uwanjani.
Manji amelalamikia pia bodi hiyo ya ligi ambayo iko kwa mpito kabla ya kufanyika kwa uchaguzi akisema haina mjumbe hata mmoja kutoka klabu ya Yanga.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.