Tuesday, July 16, 2013

Baada ya kutoroka kwenye kambi ya Starz,rungu la TFF kumuangukia Kazimoto


Shirikisho la kabumbu nchini TFF limesema litamuadhibu kiungo wa Wekundu wa Msimbazi Simba Mwinyi Kazimoto kwa kutoroka kwenye kambi ya timu ya Taifa Taifa Starz.

Katibu mkuu wa TFF Angetile Osiah amesema TFF hawana taarifa za alipokwenda Kazimoto zaidi ya kusikia kuwa amekwenda kusaka timu nchini Qatar,kitendo ambacho wanachukulia kama utovu wa nidhamu.

Angetile amesema Kazimoto amevunja kanuni za kambi ambazo anazifahamu na wachezaji wote wa Taifa Starz wanafahamu kanuni hizo ambazo wanapewa wanapoingia kwenye kambi ya timu ya Taifa.

Kazimoto ataadhibiwa kulingana na kanuni hizo za kambi na TFF imesema haitafumbia macho vitendo kama hyivyo vya utovu wa nidhamu.

Itakumbukwa kwenye msimu uliopita wa ligi kuu ya Tanzania bara Kazimoto alisimamishwa na timu yake ya Simba kwa utovu wa nidhamu kabla ya baadaye kurejeshwa kundini.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.