Tuesday, July 30, 2013

FC Lupopo mguu sawa kuondoka na Kaseja

Timu ya FC Lupopo ya Congo DRC wapo hatua chache kumnasa golikipa namba moja na nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Starz Juma Kaseja.

Mabosi wa Lupopo wapo hapa nchini tayari kumalizana na Kaseja ili akaanze kuitumikia timu hiyo katika ligi ya Congo.

Lupopo wapo tayari kutoa dau ambalo linatakiwa na golikipa huyo aliyedumu na kuibeba Simba kwa zaidi ya miaka 10 akiwa namba moja na kwenye kikao cha leo na kipa huyo ni kukubaliana baadhi ya mambo ambayo Kaseja ameyataka ili yawekwe kwenye mkataba na kumalizana.
Kaseja mwenyewe anasema baada ya mazungumzo hayo ya leo ndio atajua kama atakwenda kucheza kwenye timu hiyo au ataachana nao japo amekiri kuwa dau ni zuri ambalo limetolewa na timu hiyo na kilichobaki ni kutazama maslahi yake zaidi kama mchezaji.
Kama Kaseja akimalizana na Lupopo kwa makubaliano ya kwenda kucheza huko Congo,atakutana na washambuliaji wa Tanzania wanaocheza Tp Mazembe Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu.

Mkataba wa Simba na Kaseja umemalizika na Simba wamesema kuwa hawana mpango wa kumuongeza mkataba mpya.

KUTOKA Supermariotz blog : Kaseja nabii hakubaliki kwao,bado una kiwango cha juu na kwa umri wako sasa ndio umekomaa na ni wakati wako wa kwenda kupata changamoto mpya kwenye ligi na wachezaji usiowafahamu,kila la kheri.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.