Saturday, July 20, 2013

Sitta,Malikia wa nyuki,Sumaye wachomoza mkutano mkuu Simba

Waziri wa bunge la Africa Mashariki Samuel Sitta ametangazwa kuongezwa kwenye baraza la wadhamini wa klabu hiyo akichukua nafasi ya Sykes aliyefariki dunia.

Sitta amepata baraka zote za wanachama wa klabu ya Simba ambao wamebariki uteuzi huo kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa klabu hiyo uliofanyika leo kwenye ukumbi wa bwalo la maafisa wa Polisi Oysterbay.

Mbali na kumpitisha Sitta pia mkutano mkuu umewatangaza Rahma Al Kharoos,Cresentius Magori,Profesa Philemoni Sarungi na waziri mkuu wa zamani Fredrick Sumaye kuwa walezi wa klabu.
Aidha wanachama wa Simba waliokutana leo kuzungumza mambo ya klabu yao wamepitisha mpango mkakati wa klabu wa 2013-2018

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.