Monday, July 29, 2013

HAMILTON : Mengi makubwa yanakuja


Dereva wa magari kwenye mashindano ya Formula 1 Langalanga Lewis Hamilton amesema ushindi alioupata kwenye Hungarian Grand Prix ni mmoja wa ushindi muhimu kwenye maisha yake ya mashindano hayo.

Huo ni ubingwa wake wa kwanza tokea amejiunga na timu ya Mercedes,pia ni ushindi wake wa kwanza tokea aliposhinda kwenye United Grand Prix mwezi November.
 

Hamilton anasema ana furaha kubwa kushinda na anaamini mengi makubwa yatafuata baada ya ushindi huo uliofungua njia akiwa na Mercedes.

Kabla ya mashindano hayo Hamilton alikuwa na hofu ya kushindwa kwasababu ya ubora wa matairi lakini baada ya ushindi anasema kama tairi zitaendelea kuwa na ubora huo wanaweza kufanya vizuri kokote.

World championship standings

1 Sebastian Vettel Red Bull 172 points
2 Kimi Raikkonen Lotus 134
3 Fernando Alonso Ferrari 133
4 Lewis Hamilton Mercedes 124
5 Mark Webber Red Bull 105

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.