Friday, July 12, 2013

Muuaji wa Starz atua Swansea

Muuaji aliyetupia bao la nne la timu ya taifa ya Ivory Coast dhidi ya timu ya Taifa ya Tanzania kwenye mchezo wa kuisaka tiketi ya fainali za kombe la dunia uliopigwa uwanja wa Taifa June 16 Willfried Bony ametua Swansea City ya Uingereza.


Bony ametua kwenye timu hiyo kwa dau la paundi milioni 12 akitokea Vitesse Arnhem ya Uholanzi.

Mshambuliaji huyo itakumbukwa alizamisha bao la nne wakati Ivory Coast ilipoichapa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Starz kwa mabao 4-2 kwenye mchezo wa kuisaka tiketi ya fainali za kombe la dunia.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.