Tuesday, July 30, 2013

Mourinho bado anamuota Drogba

Bosi wa CHELSEA Jose Mourinho bado anaendelea kuonesha kuwa anatamani kuungana tena na Didier Drogba huko Stamford Bridge akiwa kama kocha au kama mchezaji.



Drogba, ambaye amebakiza mwaka mmoja kumaliza mkataba wake na Galatasaray,alikuwa kipenzi cha mashabiki huko darajani na anakumbukwa kwa kutumbukiza wavuni penati ya mwisho iliyowapa Chelsea ubingwa wa Ulaya kwenye fainali waliyocheza dhidi ya Bayern Munich.


Drogba mwenye miaka 35 aliitumikia The Blues kwa miaka 8 na Mourinho bado anaendelea kutamani huduma ya mshambuliaji huyo.


Mourinho anasema anafikiri iko siku atarejea Chelsea kwakuwa ni mchezaji muhimu kwenye historia ya klabu hiyo na siku zote ataendelea kubakia kwenye kumbukumbu za mashabiki,uongozi,mmiliki na wachezaji wenzake.
Drogba ametumbukia wavuni mara tano kwenye ligi ya Uturuki.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.