Wednesday, November 27, 2013

Ancelotti akiri kutaka "kuua"mchezaji


Boss wa zamani wa Chelsea Carlo Ancelotti amekiri kuwa alitamani kumuua mmoja wa wachezaji huko Stamford Bridge.

MTALIANO huyo aliyeiongoza Chelsea kupata mataji mawili Ligi kuu na kombe la FA katika msimu wake wa kwanza huko Magharibi mwa London lakini akatimuliwa mwaka mmoja baadaye.
Lakini wakati Ancelotti anafurahia mahusiano mazuri na wachezaji wakati akiwa the Blues, AC Milan, Paris Saint-Germain na sasa Real Madrid,anakiri kuwa kuna mchezaji mmoja ambaye hakutaka kumtaja ambaye anasema ni tatizo kubwa Stamford Bridge.

Anasema hakuwahi kuwa na matatizo na wachezaji lakini yupo mmoja hakuonesha heshima na alijaribu kummaliza lakini haikuwezekana.
Ancelotti hakutaka kumtaja mchezaji huyo japo anasema aliwahi pia Didier Drogba kwa kuchelewa baada ya kufika dakika 30 kabla ya mechi kuanza na akamuweka benchi lakini anasema mahusiano yao yaliimarika.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.