Thursday, November 7, 2013

Chelsea mguu sawa,Etoó akifanya yake

Samuel Eto'o amepasia wavuni mara mbili Chelsea ikiendelea kujikita kileleni mwa kundi E la Champions League baada ya kuishinda Schalke 04 mabao 3-0.

Schalke walianza vizuri mchezo huo wakikosa kosa kupitia kwa Julian Draxler na Adam Szalai lakini Chelsea wakatangulia kufunga baada ya mpira uliopigwa na golikipa Timo Hildebrand kugongwa na Eto'o na kutumbukia wavuni.

 Eto'o akatupia bao la pili akimalizia kazi nzuri ya kiungo MBrazil  Willian ambaye nyota yake ilingára katika mchezo huo kabla ya Demba Ba kumalizia kazi akitupia bao la tatu.



Ushindi huo kwa Chelsea unawafanya kujitawala kileleni kwa tofauti ya pointi tatu na kuendelea kuongoza kundi E na sasa wanahitaji sare katika mchezo unaofuata dhidi ya FC Basel ili kujihakikishia nafasi ya kucheza hatua ya mtoano.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.