Thursday, November 21, 2013

Chelsea,Man U zatiana pembe kumnasa kinda wa miaka 8


Chelsea na Manchester United wanatiana pembe kumuwania kinda wa miaka nane wa Argentina.

Real Madrid, Barcelona, Milan na Atletico Madrid pia zinafuatilia kwa karibu maendeleo yake akionekana ni kama Lionel Messi wa baadaye.

Kinda huyo Claudio Gabriel Nancufil,amepewa jina la utani la Snow Messi,na anachezea kwenye timu ya watoto ya Bariloche ya Argentina.

Nancufil anaelezewa kuwa ni mwenye uwezo mkubwa wa kukokota mpira na uwezo wa kumiliki mpira na kucheza nao akitumia mguu wa kushoto na pia ni mdogo kwa umri wake kuanza kufananishwa na Messi.

Familia yake tayari imempata wakala ambao ni Sueno Comunicaciones,kuzuia mpango wa kinda huyo kwenda Ulaya wakati vilabu vitano vikubwa vikihitaji huduma yake.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.