Friday, November 22, 2013

Simunic alimwa faini kwa unazi



Beki wa Croatia Josip Simunic amepigwa faini ya dola 2,600 kwa ubaguzi baada ya kuwaongoza kwa kipaza sauti mashabiki kuimba nyimbo zilizokuwa zikitumiwa na utawala wa kinazi wakati wa vita ya pili ya dunia.

Simunic mwenye miaka 35 amepinga kuhusisha suala hilo na siasa wakati alipotumia kipaza sauti kuwaongoza kwa pamoja mashabiki kuimba baada ya kuifunga Iceland na kukata tiketi ya kucheza kwenye fainali za kombe la dunia.

Fifa bado wanafikiria kama wamchukulie hatua zaidi za kinidhamu yeye binafsi na wanasubiri ripoti ya waamuzi na pia ikikusanya taarifa kutoka kwa waangalizi wa kupinga ubaguzi kwenye soka barani Ulaya.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.