Friday, November 22, 2013

Mourinho ambwatukia mkuu wa waamuzi

Boss wa Chelsea Jose Mourinho amemponda mkuu wa waamuzi Mike Riley kwa kuomba msamaha kwa West Brom kufuatia penati iliyotolewa dakika za mwisho kwenye mchezo wao dhidi ya Chelsea.

Mourinho anamini kitendo cha Riley kinaibua hatari kubwa huku akisema hakuna mtu aliyempigia simu kumuomba radhi kwa bao la pili la West Bromn ambalo mchezaji wa Chelsea Ramires alifanyiwa madhambi na Steven Reid lakini mwamuzi akaacha wakaenda kufunga.

Kocha huyo ameyasema hayo baada ya Riley kupiga simu kwa West Brom kuwaomba radhi kwa penati iliyotolewa na Andre Marriner dakika za lala salama iliyofanya matokeo kumalizika kwa sare ya kufungana mabao 2-2.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.