Friday, November 15, 2013

Ronaldo v Zlatan wanaume hawa ndio wataamua mechi ya kombe la dunia leo Portugal v Sweden

Wakiwa na mabao 48 na hat-tricks 7 kati yao Cristiano Ronaldo na Zlatan Ibrahimovic watakuwa wakitupiwa jicho ili kuziwezesha nchi zao kushiriki kwenye fainali za kombe la dunia nchini Brazil mwakani.

Na ni mmoja tu kati yao ndiye atakayeonekana kwenye fainali hizo baada ya michezo miwili ya hatua ya mtoano kuisaka tiketi ya fainali za kombe la dunia.

Ronaldo anayeichezea Real Madrid mwenye miaka 28,ana matumaini ya kuipeleka Ureno kwenye fainali za dunia kwa mara ya sita wakati Ibrahimovic mwenye miaka 32 anayeichezea Paris St-Germain ana lengo la kuipeleka Sweden kwenye fainali za kombe la dunia kwa mara ya tatu baada ya kukosa fainali za dunia 2010 nchini Africa Kusini.

Hat trick za Ronaldo 2013-14

09 Nov, La Liga: Real Madrid 5-1 Real Sociedad
30 Oct, La Liga: Real Madrid 7-3 Sevilla
17 Sept, Champions League: Galatasaray 1-6 Real Madrid
06 Sept, World Cup qualifier: Northern Ireland 2-4 Portugal

Hat trick za Ibrahimovic 2013-14

09 Nov, Ligue 1: Paris St-Germain 3-1 Nice
23 Oct, Champions League: Anderlecht 0-5 Paris St-Germain (scored four)
14 Aug, Friendly: Sweden 4-2 Norway

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.