Thursday, November 21, 2013

Fifa yambeba Ronaldo tuzo ya Ballon d’Or


FIFA imetangaza kuongeza mwisho wa upigaji kura za kuwania tuzo ya Ballon d’Or 2013 mpaka November 29.

Maamuzi hayo huko Hispania yamechukuliwa ni kama ya kumbeba Cristiano Ronaldo dhyidi ya wapinzani wake kama Lionel Messi, Franck Ribery na Zlatan Ibrahimovic,baada ya nahodha huyo wa Ureno kupiga hat trick dhidi ya Sweden na kuipa tiketi timu yake ya Taifa kukata tiketi ya fainali za kombe la dunia 2014.

Mwisho wa makocha,manahodha na waandishi wanaopiga kura hizo kuwasilisha majina matatu ya juu ilikuwa November 15,saa kadhaa baada ya kumalizika kwa michezo ya hatua ya mtoano na Rebery anayecheza Bayern Munich alikuwa akipewa nafasi zaidi ya kuibuka na ushindi wa tuzo hiyo.

Na sasa tarehe imesogezwa mpaka Ijumaa ya November 29 na kura zinaweza kubadilika na kuelekea kwenye kiwango cha sasa kama alichokionesha Ronaldo hatua inayoonekana kumbeba zaidi mshambuliaji huyo anayepigiwa chapuo kuibuka na tuzo hiyo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.