Monday, November 11, 2013

Hawa wanaweza kupishana na Joe Hart Man City


Kipa namba moja wa England Joe Hart ambaye katika mchezo wa jana alipigwa benchi na timu yake ya Manchester City chini ya Manuel Pellegrini baada ya mlolongo wa makosa na lango kukabidhiwa MRomania Costel Pantillimon shaka imeongezeka ya kuondolewa kabisa kikosini na nafasi yake kuchukuliwa na golikipa wa Barcelona Victor Valdes.
Valdes mwenye miaka 31,anaondoka Barca mwishoni mwa msimu na anataakiwa pia na Monaco lakini City wako tayari kumpigania.

Japo kipa wa QPR raia wa Brazil Julio Cesar, 34, anatajwa kwenye mipango ya City, pamoja na makipa wawili waliowahi kuwa chini ya Pellegrini Wilfredo Caballero wa malaga na yule wa Real Madrid Iker Casillas.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.