Monday, November 25, 2013

AVB : Spurs kupigwa sita aibu yetu wenyewe


Kocha wa Tottenham Andre Villas-Boas amesema kikosi chake kinatakiwa kuona aibu kwa kipigo cha mabao 6-0 kutoka kwa Manchester City.

Spurs imekubali kipigo kikubwa kwa mara ya kwanza tokea ilipofungwa 7-1 na Newcastle December 1996.

Kipigo hicho cha jana kimewaacha Spurs kukalia katika nafasi ya tisa wakiwa na point inane nyuma ya wanaoongoza ligi Arsenal.

Villas-Boas amesema kipigo walichokipata ni kikubwa na ambacho wanatakiwa kuona aibu wao wenyewe kwa kukosa umakini na kuruhusu kipigo kikubwa ambacho hawakustahili.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.