Thursday, March 27, 2014

Valdes kulikosa kombe la dunia

Golikipa wa Barcelona na Spain Victor Valdes atakosa fainali za kombe la dunia baada ya kuumia goti.

Kipa huyo alitolewa kwa machela mapema hapo jana kwenye mchezo ambao Barcelona ilipata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Celta Vigo.

Barcelona wamethibitisha kuwa kipa huyo anahitaji upasuaji.

Valdes tayari ametangaza kuondoka kwenye klabu hiyo ifikapo mwishoni mwa msimu.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.