Tuesday, March 11, 2014

KUFURU : Ronaldo awaburuza wanasoka duniani kwa utajiri

Mshambuliaji wa Ureno na Real Madrid Cristiano Ronaldo anaelezwa kuwa mwanasoka tajiri zaidi duniani kwasasa kwa wale ambao bado wanacheza.

Mchezaji huyo bora wa dunia amempiga chini nyota wa Argentina na Barcelona Lionel Messi katika orodha hiyo ya wachezaji matajiri akikusanya kitita cha paundi milioni 148.

Nyota aliyestaafu David Beckham ndiye alikuwa kinara wa utajiri kwa mwaka jana 2013 lakini tokea alipostaafu soka kwasasa hana kigezo cha kuingia kwenye orodha hiyo inayoshirikisha wachezaji ambao bado wanacheza.

Messi yupo kwenye nafasi ya pili akiwa anaingiza kiasi cha paundi milioni 146 akifuatiwa na Eto'o anayeingiza paundi milioni 85 wakati Wayne Rooney yeye anaingiza paundi milioni 84 na Kaka anakamilisha tano bora akikusanya kitita cha paundi milioni 82.

Orodha hiyo ni kwa mwaka husika na hauhusiani na miaka iliyopita.

Shuka na 10 bora ujionee.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.