Tuesday, March 25, 2014

KISA KESI YA MTOTO WAKE : Mahakama yamvua cheo Bosi wa Cricket India


Mahakama kuu nchini India imemtaka boss wa juu wa cricket kuachia nafasi yake ili kupisha uchunguzi wa haki katika madai ya upangaji matokeo kwenye ligi kuu ya India.

Jopo la majaji wawili limesema Rais wa bodi inayoendesha cricket nchini humo Narayanaswami Srinivasan amekuwa akichelewesha uchunguzi ambao unamuhusisha motto wake wakambo.

Mahakama hiyo imesema kama Srinivasan anayetajwa kama mmoja wa watawala wenye nguvu duniani kwenye mchezo huo hatajiuzulu katika nafasi yake hiyo wataamuru aondolewe.

Alichaguliwa kama mwenyekiti wa cricket duniani,baraza la kimataifa la cricket mwezi February na ataanza kazi hiyo mwezi July.

Mtoto wa kambo wa Srinivasan ,Gurunath Meiyappan, alihusishwa na upangaji wa matokeo mwezi uliopita.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.